Inahuzunisha Sana..Mke Ammwagia Mafuta ya Moto Mume na Mtoto Baada ya Kupewa Talaka (Video)

0

Mohamed Maulid mkazi wa Pugu Kinyamwezi ambaye ni mfanyakazi wa Tanesco na mtoto wake Sumaiya Mohamed (3), wamemwagiwa mafuta ya moto na mke wake (Severine) baada ya mke huyo kupewa talaka siku mbili kabla ya tukio hilo.
Maulid alisema baada ya kumpa mwanamke huyo talaka alikuwa anampiga tu tarehe kuwa ‘ntaondoka kesho, ntaondoka kesho.’ “Na nilivyokuwa naenda kazini nilimuuliza utaondoka saa ngapi akasema ataondoka jioni, nikahisi kwamba anaona aibu kuondoka mchana ataondoka jioni,” amesimulia.
“Nilikuwa nimelala nikasikia kama moto umelipuka, nilikuwa nimelala fofoFo, nikashtuka nikaanza kupiga kelele nimemwagiwa maji ya moto nikapiga kelele majirani wengine wakanisikia wakatoka nje, wakaenda kumuangalia na mtoto wakakuta na mtoto naye kaungua sana na yupo kule wodi ya watoto.”
Baadaye majirani wakanisaidia wakamuita dereva taksi nikawaambia nikimbizeni hospitali kwa uzima wangu. Mimi nilipomwagiwa mafuta yale, nilikurupuka nikakuta mlango upo wazi na wakati mlango nilikuwa nimefunga nimefunga na misumari kwasababu nilikuwa simuamini tena kwanini hataki kuondoka, nikakuta mlango ule umefunguliwa na wa nyuma umefunguliwa na mtoto wangu alimwagiwa mafuta kichwani nilimuona.”
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.