Mohamed Maulid mkazi wa Pugu Kinyamwezi ambaye ni mfanyakazi wa Tanesco
na mtoto wake Sumaiya Mohamed (3), wamemwagiwa mafuta ya moto na mke
wake (Severine) baada ya mke huyo kupewa talaka siku mbili kabla ya
tukio hilo.
Maulid alisema baada ya kumpa mwanamke huyo talaka alikuwa anampiga tu
tarehe kuwa ‘ntaondoka kesho, ntaondoka kesho.’ “Na nilivyokuwa naenda
kazini nilimuuliza utaondoka saa ngapi akasema ataondoka jioni, nikahisi
kwamba anaona aibu kuondoka mchana ataondoka jioni,” amesimulia.
“Nilikuwa nimelala nikasikia kama moto umelipuka, nilikuwa nimelala
fofoFo, nikashtuka nikaanza kupiga kelele nimemwagiwa maji ya moto
nikapiga kelele majirani wengine wakanisikia wakatoka nje, wakaenda
kumuangalia na mtoto wakakuta na mtoto naye kaungua sana na yupo kule
wodi ya watoto.”
Baadaye majirani wakanisaidia wakamuita dereva taksi nikawaambia
nikimbizeni hospitali kwa uzima wangu. Mimi nilipomwagiwa mafuta yale,
nilikurupuka nikakuta mlango upo wazi na wakati mlango nilikuwa
nimefunga nimefunga na misumari kwasababu nilikuwa simuamini tena
kwanini hataki kuondoka, nikakuta mlango ule umefunguliwa na wa nyuma
umefunguliwa na mtoto wangu alimwagiwa mafuta kichwani nilimuona.”

Please do not enter any spam link in comment box